Brighton, Leicester, Roma na Lyon zamuwania Samatta


Mbwana SamattaHaki miliki ya pichaGETTY IMAGES
downoad app ya MIKOGO BLOG playstore kupata taarifa zaidi 
Klabu ya Brighton inayocheza ligi ya Primia ya England inaongoza msururu wa klabu zinazomuwania mshambuliaji wa Tanzania, Mbwana Samatta.
Klabu nyengine za England ambazo zinamuwania Samatta ni Aston Villa, Watford, Leicester na Burnley.
Kwa mujibu wa gazeti la The Sun la Uingereza Samatta ana thamani ya Pauni milioni 12.
Samatta ambaye bado ana mwaka mmoja kwenye mkataba wake na mabingwa wa Ubelgiji KRC Genk pia amezivutia klabu za Roma ya Italia na Lyon ya Ufaransa.
Mshambuliaji huyo ambaye aliongoza kwa kupachika mabao msimu uliopita nchini Ubelgiji ameweka wazi kuwa anataka kuelekea nchini England msimu ujao.
"Kwa sasa hivi siwezi kusema sana, ni kitu ambacho kipo kwenye mchakato nasubiria kitakapokuwa tayari na wakati utakapofika nitaweza kukizungumza. Lakini sijioni tena Genk, namuomba Mwenyezi Mungu litimie, lakini ikishindikana bado nina mkataba na Genk," aliiambia runinga ya Azam TV ya Tanzania wiki iliyopita.
chanzo: bbc

Comments