Yanga kuivaa Ruvu Shooting Jumatatu




Baada ya mchezo dhidi ya Biashara United jana, kikosi cha Yanga kinarejea jijini Dar es salaam tayari kwa mchezo unaofuata dhidi ya Ruvu Shooting

Mchezo huo utapigwa Jumatatu, May 13 katika uwanja wa Uhuru

Baada ya kupoteza mchezo wa jana, Yanga ni kama haina nafasi ya kutwaa ubingwa msimu huu, kilichobaki ni kukamilisha ratiba tu

Kihamesabu, Simba inahitaji kushinda michezo mitatu tu ili iweze kutetea ubingwa, huku wakiwa na michezo sita ya viporo

Baada ya mchezo wa Ruvu Shooting, mchezo utakaofuata ni dhidi ya Mbeya City kisha kumaliza msimu kwa kuumana na Azam Fc

Kocha Mwinyi Zahera amewashukuru mashabiki wa timu hiyo kwa sapoti waliyotoa tangu mwanzoni mwa msimu na ameahidi msimu ujao watarejea wakiwa imara zaidi

Comments