Katika mchezo huo mabao ya Simba yalifungwa na Bocco mawili, Kagere na Chama kila moja lifunga bao moja
Dar es Salaam. Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi Simba, Mohammed Dewji 'Mo Dewji' ameshindwa kujizuia kwa kushangilia kwa nguvu wakati vijana wake wakichapwa mabao 4-5 na Sevilla kwenye Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam.
Mo Dewji alishinda kujizuia ni baada ya kufungwa bao la tatu na John Bocco aliyepokea pasi kutoka kwa Meddie Kagere.
Mo Dewji aliyekuwa ameketi karibu na Mkurungezi wa Utawala na Udhibiti wa Sportpesa, Abbas Tarimba alianza kushangilia kwa nguvu huku akirukaruka baada ya Simba kupata bao la tatu.
Mo Dewji alikuwa amesimama huku akirukaruka na kumpa mkono wa pongezi Tarimba.
Baada hapo Mo Dewji alikaa chini huku akionekana bado kuwa na furaha akiwapa mkono wa pongezi waliokuwa karibu yake.
Mo Dewji hakushngilia bao hilo peke yake kwa upande wa viongozi waliokuwa hapa jukwaa Kuu ni Mtendaji Mkuu wa Simba, Magori, Mwenyekiti Swedy Mkwabi.
Wengine Hussein Kita, Mulamu Ng'ambi, Mwina Kaduguda wote na Wajumbe wa Bodi, bila kumsahau Ofisa habari wa Simba, Haji Manara aliyekuwa amekaa karibu na wanamitindo Hamisa Mobeto.
Comments
Post a Comment