BBC imeripoti kuwaTaifa la Tanzania linaongoza kwa idadi ya watu wanaovuta bangi katika eneo la Afrika mashiriki.
Kulingana na utafiti wa watumizi wa marijuana uliofanywa na shirika la New Frontier Data kutoka Uingereza, Tanzania ambayo iko katika nafasi ya tano kwa idadi ya watumizi wa mmea huo barani Afrika, inaongoza eneo la Afrika mashariki ikiwa na watu milioni 3.6 wanaotumia bangi ikifuatiwa na Kenya ambayo iko nafasi ya sita na watu milioni 3.3 na Uganda katika nafasi ya nane ikiwa na watumizi milioni 2.6.
Mataifa yanayoongoza kwa uvutaji wa bangi barani Afrika ni Nigeria ilio na watumiaji milioni 20.8, ikifuatiwa na Ethiopia yenye watu milioni 7.1, Misri watu milioni 5.9 huku taifa la DR Congo likiwa la 4 na watu milioni 5.
Mataifa ya Burundi na Sudan Kusini hayakuorodheshwa.
Lakini taifa la Sudan linashikilia nafasi ya 7, ilikiwa na watumizi milioni 2.7, likifuatiwa na Madagascar lenye watu milioni 2.1, Ghana milioni 2, Msumbiji watu milioni 1.9, na Angola watu milioni 1.8.
Mataifa ya Afrika yalio na watumizi wa wachache wa bangi kulingana na ripoti hiyo ya 2019 ni pamoja na Zimbabwe ilio na watu milioni 1.1, Malawi watu milioni 1.2, Niger watu milioni 1.2 na Zambia watu milioni 1.4
Ripoti hiyo inajiri siku chache tu baada ya Mbunge wa Kahama mjini nchini Tanzania, Jumanne Kishimba kutoa wito kwa serikali kuhalalisha matumizi ya mmea huo kwa mautumizi ya dawa.
Akizungumza bungeni aliyataja mataifa mengine manne ya Afrika ambayo tayari yemahalalisha Marijuana kutumiwa kutengeneza dawa.
Kulingana na gazeti la The Citizen nchini Tanzania mbunge huyo anasema kuwa ni vyema kama taifa kuanza kufikiria kuhusu fursa hiyo mapema.
Hivi majuzi rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli alinukuliwa akimtaka waziri wa maji na umwagiliaji Profesa Makame Mbarawa kuwa mkali kusimamia miradi ambayo imekusudiwa na serikali.
''Zinazungumzwa fedha zimeenda kwenye miradi lakini hazikwenda, kuna wakati nilienda kanda ya ziwa ninauliza mradi wa maji uko wapi zimetumika milioni 400 zilikua milioni 800 lakini maji hayapo''
''Sasa nikuombe waziri na watendaji wako mkawe wakali kweli kweli kama una uwezo wa kuvuta bangi ya njombe ili uwe mkali kaivute, kaivute kisirisiri ili wasikuone ukiivuta ili ukienda kwenye mradi hawa mainjinia wa maji wakafanye kazi''.Alisema Rais Magufuli
Nchini Tanzania ni haramu kuvuta bangi na ukiukaji wa sheria hiyo inavutia hukumu kali jela na faini kubwa.
Serikali ya Tanzania imepinga uwezekano wowote wa kuhalalishwa kwa mmea huo katika taifa hilo.
Hatahivyo takwimu mpya za Shirika la New Frontier Data zinakadiria jumla ya masoko ya bangi yalio halali na yasiokuwa halali yanayaouza bangi barani Afrika kuwa dola 37.3b (juu ya Shs139.2 trilioni), na kushuka kwa wastani kati ya $ 18.99b na $ 63.7b.
Bangi hutumika sana barani Afrika huku kukiwa na kiwango cha wastani cha kila mwaka cha asilimia 11.4 kati ya watu wazima wenye umri wa kati ya 15-64, ikikaribia kuwa mara mbili ya kiwango kinachotumika duniani cha asilimia sita ,ripoti hiyo inasema.
Makadirio hayo ya utumizi wa mihadarati yanatokana na data zilizopo kutoka kwa vitengo vya serikali na mashirika ya afya ya umma duniani.
Hatahivyo makadirio hayo hubadilika kila data mpya zinazpopatikana.
Mataifa mengine yamehalalisha utumizi wa bangi kwa namna fulani huku mataifa mengine kama Uganda yakiwa katika awamu ya kwanza kutengeneza kanuni zao za masoko.
Huku serikali, wafanyabiashara, maafisa wa afya, na wataalam wa kisheria wakifanya kazi ya kuweka misingi ya masoko mapya ya kisheria kote ulimwenguni, ripoti hiyo inasema kuwa ni muhimu kuelewa ukubwa wa fursa za soko na wanaoshawishi ukuaji wa sekta hiyo.
Mahitaji ya kila mwaka ya bangi duniani yanakadiriwa kuwa $334.4b katika kipindi chote cha mwaka 2018.
Makadirio ya thamani ya mahitaji ya mmea huo hutegemea kiwango kinachotumiwa na kila nchi kwa kila mtumizi na bei yake.
Mwaka wa 2015, Uganda ilianzisha sheria ya mihadarati na Dawa za Kisaikolojia ambayo inaruhusu kilimo, uzalishaji na usafirishaji wa bangi inayotumika kwa matibabu.
Serikali ya taifa hilo imetoa leseni kwa kampuni ya Industrial Hemp (U) Ltd kukuza na kuuza nje bangi ya matibabu kwa madhumuni ya matibabu.
Kampuni ya Hemp (U) Ltd ilianzishwa mwaka 2012 na kwa sasa hufanya kazi ikishirikiana na kampuni ya Pharma Limited, mojawapo ya makampuni makubwa ya marijuana nchini Israeli kwenye soko la hisa la Tel Aviv
Wamewekeza $ 360m katika sekta ya bangi na kuanzisha mashamba ya bangi katika Wilaya ya Hima, Kasese.Sehemu mbalimbali duniani mtazamo kuhusiana na matumizi ya mmea wa cannabis yaani bangi unabadilika kwa kasi.
Serikali mpya ya Mexico ina mpango wa kuhalalisha matumizi ya bangi kama njia ya kujiburudisha, sawa na ilivyofanya utawala mpya wa Luxembourg. Wakati huo huo, viongozi wakuu nchini New Zealand, wanakusudia kuandaa kura ya maoni ya namna watakavyoshughulikia swala hilo.
Jinsi maoni ya umma - na yale ya serikali- yanavyobadilika, ni dhahiri kuwa mataifa mengi yatafuata mkondo huo. Maswali yanayoibuka ni kwa namna gani nchi hizo zitadhibiti matumizi na usambazaji wa mmea huo?
Ni nini hasa kinachopelekea mataifa mbalimbali katika kulegeza kamba kwenye sheria zake, au hata kuamua kuidhinisha ,matumizi ya bangi moja kwa moja?
Comments
Post a Comment