AJIBU KWENDA TP MAZEMBE

TP Mazembe itamsajili kiungo wa Yanga Ibrahim Ajib Migomba akitarajiwa kujiunga na timu hiyo Julai 01 2019


TP Mazembe imeiandikia barua Yanga kuitaarifu juu ya nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo.


Mazembe itamsajili Ajib baada ya kumaliza mkataba na Yanga


Aidha TP Mazembe imeiomba Yanga impe ruhusa ya siku tatu wiki hii ili aweze kwenda Congo kukamilisha taratibu za usajili


Hii ni habari njema kwa Ajib ambaye msimu huu umekuwa mzuri sana kwake


Ajib ameifungia Yanga mabao sita na kutengeneza mabao 17 kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara inayoelekea ukingoni




Comments