TP Mazembe itamsajili kiungo wa Yanga Ibrahim Ajib Migomba akitarajiwa kujiunga na timu hiyo Julai 01 2019
TP Mazembe imeiandikia barua Yanga kuitaarifu juu ya nia ya kutaka kumsajili kiungo huyo.
Mazembe itamsajili Ajib baada ya kumaliza mkataba na Yanga
Aidha TP Mazembe imeiomba Yanga impe ruhusa ya siku tatu wiki hii ili aweze kwenda Congo kukamilisha taratibu za usajili
Hii ni habari njema kwa Ajib ambaye msimu huu umekuwa mzuri sana kwake
Ajib ameifungia Yanga mabao sita na kutengeneza mabao 17 kwenye ligi kuu ya Tanzania Bara inayoelekea ukingoni
Comments
Post a Comment